MTANGAZAJI

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA CHATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI





Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Dk. Helen Kijo-Bisimba (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari  kwenye mafunzo ya siku mbili ya waandishi wa habari kuhusu haki za wanawake kwenye Katiba, ushiriki wa vyombo vya habari kwenye mabaraza ya Katiba na haki ya kupata habari, kulia ni Mratibu wa Katiba wa kituo hicho, Anna Henga


 


         Mwandishi wa Habari ,Amosi Aloyce akichangia mada.





 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk.Helen Kijo-Bisimba  amesema Katika Katiba mpya ni muhimu kuwekwa kipengere cha haki za wanawake ili kulisaidia kundi hilo.

Kauli hiyo aliitoa katika mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari kuhusu haki za wanawake kwenye Katiba, ushiriki wa vyombo vya habari kwenye mabaraza ya Katiba na haki ya kupata habari yaliyomalizika leo katika ofisi za kituo hicho kilichopo kijitonyama,
Dar es Salaam.

Alisema katika Katiba ya sasa hakuna kipengere chochote kinachoelezea haki za wanawakwe mbali ya ibara ya 12 kutamka usawa wa binadamu.

Alisema kila mwanamke ana haki ya kuheshimiwa utu wake na kulindwa dhidi ya mila potofu na ubagunzi wa kijinsia.
 

Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo zimeridhia mikataba ya kimataifa mbalimbali ambazo zinawalinda wanawake kwa namna moja au nyingine.
 

Tafiti za kituo hicho zinaonesha kuwa  kumekuwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia kama vilivyoainishwa kwenye Tamko la Umoja wa Mataifa la uondoaji wa Ukatili dhidi ya wanawake la mwaka 2005.
 

Ukatili huo  ni kitendo chochote cha ukatili kuhusu jinsia, ambacho kinaweza kusababisha madhara, maumivu ama mateso ya kimwili au kisaikilojia kwa mwanamke, ikiwa ni pamoja na vitendo vya kutishia,kulazimisha, kunyima uhuru, bila kujali vimefanywa ama kwenye kadamnasi.

Mratibu wa Katiba wa Kituo hicho Anna Henga alisema ni wakati muafaka wa kuingiza kipengere hicho katika Katiba mpya tunayoitarajia kuipata.

Takwimu zilizotolewa katika mafunzo hayo zinaonesha kuwa kuna umuhimu wa nafasi za wabunge wa viti maalumu kwani wamefanikiwa kuchangia  maswali ya nyongeza katika vikao vya bunge kwa asilimia 50 licha ya idadi yao kuwa chini ya 40.

Picha zote na Mwaibale blog

1 comment

Anonymous said...

WATANZANIA WENGI NI MBUMBUMBU KWENYE SUALA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA NILITEGEMEA KITUO HIKI KINGEEGEMEA ZAIDI KATIKA KUWAELIMISHA WATANZANIA CHA AJABU NI KITUO HIKI KUFANYA KAZI KAMA CHAMA CHA SIASA KISICHOKUWA NA USAJIRI NILITEGEMEA KINGEKUWA REFA ANAYEKEMEA PANDE ZOTE ZINAZOVUNJA HAKI ZA BINADAMU BADALA YAKE NI UCHOCHEZI NA KUWAHAMASISHA WATANZANIA WAVUNJE SHERIA HALALI WAKATI FULANI HAYATI NYERERE ALISEMA TUNAHITAJI MAPINDUZI KUONDOKANA NA UKOLONI NA UKOLONI MAMBOLEO WAKASHINDWA KUMUELEWA NCHI NYINGI ZA KIAFRIKA ZIKAANZA KUPINDULIWA ILIBIDI ATOE AINISHO JIPYA KUWA HAYO SIO MAPINDUZI BALI NI MAASI KUHAMASISHA WATANZANIA WAONDOE SERIKALI HALALI ILIYOCHAGULIWA KIDEMOKRASIA SI UKOMBOZI NI UASI LAZIMIZA UZUIWE KWA NGUVU ZOTE MUSIVURUGE UTAWALA BORA

Mtazamo News . Powered by Blogger.