Tuesday, May 21, 2013

RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KUZINDUA MIRADI YA UJENZI WA BARABARA YA DODOMA – IRINGA

Wizara ya Ujenzi inapenda kutoa taarifa kwa Umma kwamba, Mei 22, 2013 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa miradi ya ujenzi wa barabara kama ifuatavyo:-

1)  Tarehe 22 Mei, 2013 Asubuhi kuweka jiwe la msingi sehemu ya Dodoma – Fufu Escarpment (km 93.8) katika eneo la Dodoma Mjini.


2)  Tarehe 22 Mei, 2013 Mchana kuweka jiwe la msingi sehemu ya  Fufu Escarpment – Migori (km 70.9) na Migori – Iringa (km 95.3) katika Kijiji cha Migori Wilayani Iringa Vijijini.


Barabara ya Iringa - Dodoma ni sehemu ya barabara muhimu ijulikanayo kama “Great North Road” inayoanzia Capetown Afrika ya Kusini hadi Cairo, Misri kupitia Tanzania. Nchini Tanzania inaunganisha Miji ya Tunduma (mpakani na Zambia), Mbeya, Iringa, Dodoma, Arusha na Namanga (mpakani na Kenya).


Mradi huu ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara na unalenga kupanua fursa za kiuchumi na kibiashara kwa wananchi, na kati ya Tanzania na nchi jirani za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Kwa njia hii, barabara itakuza uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.


Taarifa hii imetolewa na;

Balozi Herbert E. Mrango
 
KATIBU MKUU WIZARA YA UJENZI

Monday, May 20, 2013

UZINDUZI WA DVD MWONEKANO NAMBA MBILI YA MBIU KWAYA HUU HAPA

 

Mbiu Kwaya toka Kanisa la Waadventista Wasabato Tandale jijini Dar es salaam inataraji kufanya uzinduzi wa DVD mwonekano namba 2 waliyoipa jina la Fikiri Mwenyewe,uzinduzi utakofanyika Juni 2,2013 katika ukumbi wa Delux Hall Sinza  jijini Dar es salaam,Tanzania,kuanzia saa 6 mchana.

Uzinduzi huo uliodhaminiwa na Excellent Pro utawahusisha pia waimbaji wa Sonda ya Dilu,Kurasini SDA Choir,Angaza Kwaya,Familia ya Injili

Friday, May 17, 2013

TAMASHA LA UIMBAJI LA VOCAL PRAISE NA GOSPEL FLAMES HILI HAPA

Waimbaji wa Vocal Praise (Pichani) toka katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni Mwembechai kuanzia leo wakishirikiana na waimbaji wengine wa kanisa hilo Gospel Flames watakuwa wakifanya tamasha la uimbaji kila siku ya ijumaa kanisani hapo kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 1:30 jioni.

Hili litakuwa ni tamasha la aina yake ambapo utasikia nyimbo za injili zilizopangiliwa kiufundi na waimbaji ambao miongoni mwao ni walimu wa kwaya mbalimbali.Hii itakuwa ni changamoto hasa kwa makundi yanayoimba nyimbo za injili za aina ya acappella

Wednesday, May 8, 2013

TAMASHA LA FRIENDS OF JESUS CHOIR HILI HAPA


Friends of Jesus Choir (FoJ) ya  Rwanda  inataraji kufanya tamasha la uzinduzi wa toleo lao namba saba walilolipa jina "SHEPHERD OF MY SOUL". likiwa na nyimbo  5 za kinyarwanda , 6za kiingereza na mmoja wa kiswahili.

Waimbaji wengine watakaokuwepo ni kwenye uzinduzi huo utaofanyika kwenye Hoteli ya Serena,Kigali Rwanda Mei 18,2013 ni  The Voice toka Dar es salaam, Tanzania,Shower Power toka Zimbabawe na  Trevor toka Marekani  ambaye ni Profesa wa Muziki wa Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki na Kati cha Kanisa la Waadventista Wasabato kilichopo nchini Kenya
 

WAZIRI MKUU WA TANZANIA AMEONYA KUTOSHABIKIA MAAFA


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewaonya baadhi ya watu wanaofanya ushabiki wa kisiasa kwenye tukio la mlipuko wa Arusha na kuwataka wasitumie tukio hilo kujipatia umaarufu na badala yake watumie fursa hiyo kuwafariji walioathirika na kuwa watulivu hadi suala hilo lifikie hatma yake.
Waziri Mkuu amesema tukio hilo ni kubwa, na kitendo hicho ni kibaya kinachostahili kulaaniwa vikali kwa hiyo haifai watu wachahe kujipatia umaarufu kupitia tukio hilo.

Ametoa kauli hiyo jana asubuhi (Jumanne, Mei 7, 2013) wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwatembelea ili kuwajulia hali majeruhi waliolazwa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, jijini Arusha.

Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na hali ya utulivu wa wananchi wa Arusha na hasa waliokaribu na Kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, kufuatia mlipuko wa mabomu uliotokea Jumapili iliyopita, Mei 5, mwaka huu.
Alisema ameguswa pia na hali ya matibabu inayotolewa kwa majeruhi katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, jijini Arusha.
Waziri Mkuu alikatisha shughuli za Bunge juna mchana na kuelekea Arusha. Mara baada ya kuwasili KIA juna jioni, Waziri Mkuu alikwenda moja kwa moja Parokia ya Olasiti ili kujionea hali halisi na kuwapa pole wamunini wa Kanisa hilo.

Baadaye alikwenda kumjulia hali Askofu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu Josephat Lebulu pamoja na Balozi wa Vatican, Mhashamu Askofu Fransisko Padilla ambako alifanya nao mazungumzo na kuwahakikishia viongozi hao kwamba Serikali itafanya kila iwezalo hadi iwabane wahusika.

Akiwa hospitali ya Mount Meru leo asubuhi, Waziri Mkuu alimweleza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Dk. Frida Mokiti kuwa asisite kuwasiliana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Magesa Mulongo endapo hali ya majeruhi itabadilika na watahitaji matibabu zaidi.

Katika ziara hiyo fupi, Waziri Mkuu alikabidhi vifaa vyenye thamani ya sh. milioni 23.3 ambavyo ni dawa na vifaa tiba kwa uongozi wa hospitali hiyo ambavyo vilitolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) chini ya uhamasishaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kukabidhi misaada hiyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Bw. Lazaro Nyalandu alisema juzi (Jumatatu, Mei 6, 2013), TANAPA ilitoa mablanketi 50 hospitali hiyo na kwamba wafanyabiashara wa sekta ya utalii wa mjini Arusha wamejipanga kutoa msaada zaidi ili kuisaidia hospitali hiyo kumudu kuwahudumia majeruhi wa mlipuko huo.

Hadi sasa, watu watatu wamepoteza maisha kutokana na mlipuko huo ambapo watu wanane wamekamatwa na kuhojiwa na polisi. Kati yao, wanne ni raia wa Saudi Arabia na waliobakia ni wakazi wa Arusha. Polisi bado wanaendelea na uchunguzi wa tulio hilo.

Akitoa taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Arusha alisema wagonjwa watatu wana hali mbaya ambapo mgonjwa mmoja yuko Muhimbili na wawili wako hapo hapo Mount Meru.

“Watu 66 waliathirika na mlipuko huo, watatu wamefariki na kati ya wagonjwa 63 waliobakia, wagonjwa 24 wamesharuhusiwa kurudi nyumbani, waliobakia wanaendelea kupatiwa matibabu,” alisema.
Waziri Mkuu amerejea Dodoma mchana huu.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P 980,
DODOMA.
JUMANNE, MEI 7, 2013.

Saturday, May 4, 2013

UZINDUZI WA DVD YA RESTUTA WILLIAM MWACHULA KUFANYIKA KESHO MEI 5,2013 TAZARA DAR ES SAALAM


 Mtangazaji akiwa na Waimbaji wa Victory Singers toka Mwanza,Joseph Oola,Namsifu Makacha toka Arusha na Restuta Mwachula baada ya kipindi cha Lulu za Injili leo Morning Star Radio waimbaji hawa wataimba kesho Mei 5,2013 katika uzinduzi wa Dvd ya kwanza ya Restuta Mwachula toka Dar es salaam utakaofanyika katika ukumbi wa TAZARA barabara ya Nyerere kuanzia saa sita mchana

Waimbaji wengine watakaokuwepo kwenye uzinduzi huo ambao utachangia sh.3000 za kitanzania ni Angaza SDA Choir,Mbiu Kwaya,Ulongoni A,Acacia Singers na Sonda ya Dilu .



WANAOIFUATILIA

ZILIZOPITA

 

MTANGAZAJI. Copyright 2011 All Rights Reserved This Blog presented by ReedzSolution