Friday, November 20, 2009

APPLICATION TO PARTICIPATE IN ALAT EVENTS DODOMA 7 - 13 DEC 2009

Dear Policy Forum members,
We are pleased to invite you to apply to participate in the Annual Working Congress of the Association of Local Authorities of Tanzania (ALAT) which will take place in Dodoma, Tanzania on the 7th and 8th December 2009 as part of the Commemoration of its 25th Anniversary.
The congress will be followed by an official gathering to commemorate the 25th Anniversary of ALAT and the launching of Local Government Reform Program II (LGRP II commonly known as D by D) on 13th December 2009.
There will also be an International Workshop on 10th and 11th December which will bring together stakeholders in the local government sector in Tanzania and outside Tanzania.
Policy Forum have been invited to these events and accorded 15 spaces for members to attend and participate: our theme for participation is CSO AND LOCAL GOVERNMENT ACCOUNTABILITY :The need and opportunities.
Some members of Policy Forum have committed to assisting other members to attend these events and therefore will finance 10 of the 15 spaces
The members to be accorded this support will be selected basing on the following criteria:
-Members engaging/implementing Social Accountability Monitoring (or related strategies) in their areas focusing on Local governments,
-Those with and wish to share relevant lessons learned from implementing the Accountability Monitoring strategies
-Must be members of PF,
-First come first served.
Those who can finance their own participation will be considered separately and preferentially so that we might negotiate additional spaces. For further information please contact the undersigned at marcossy@yahoo.com or accountability@policyforum.or.tz or simply call 0712 or (0784) 417 307

Thursday, November 19, 2009

MCHONGO WA KUWASAIDIA WATOTO

Naamini kuna watu wengi walio na njozi na wanaoguswa na kuwasaidia watoto,kama ndivyo habari ni:
The International Labour Organisation, under the Joint UN Programme onMaternaland Newborn Mortality Reduction, invites proposals for the establishment ofself-help, community-based, low-cost childcare facilities for familiesworkingin the formal or informal economy in selected areas in Dar es Salaam.
Kwa maelezo zaidi tembelea blog pacha ambayo ni http://childrenafrica.blogspot.com

Wednesday, November 18, 2009

MTANDAO WA MATAPELI NI WA MUDA MREFU

 Nimeguswa na hili na kwa sababu ni 'point of pain' naomba kuwashirikisha na mimi kidogo tu kuhusu utapeli na wizi wa kimtandao. Mimi vile vile nimeingizwa mjini kupitia utapeli wa madalali wa nyumba za kupanga.

Jamaa walifika nyumbani kwangu na kuacha barua kuhusu nia ya wataalamu wa JICA kutaka kupanga nyumba etc. Ndugu zangu wakadanganyika baada ya kuona mikataba ikiwa na nembo zinazovutia. Tukatakiwa kufanya marekebisho kulingana na mahitaji ya mpangaji, na hao madalali wakajifanya wanaweza kushighulikia marekebisho hayo haraka ili kukidhi mahitaji kabla ya deadline ya kuonyesha nyumba hiyo kwa mabosi.


Unaweza kutabiri yaliyofuata lakini tuliingizwa mkenge. Jamaa hawa wanatembelea Tanzania nzima. Na tukio hili lilitokea Singida mimi mwenyewe nikiwa Mwanza.



Nimeriport jambo hili Police na nimepelekwa katika kitengo cha cybercrime. Kufuatana na utafati unaondelea tumeweza kuwatambua wahusika. Kwa vile wanatumia simu si vigumu kuwapata hata kama wakibadilisha line.



Kilichonistua ni kwamba jamaa wa mtandao huu wameanza shughuli hizi tokea 2003. Modus Operandi ni ile ile na wanatumia majina yale yale. Kufuatana na utafiti tuliofanya wamewahi kuwaibia watu wa aina zote - makasisi, watawa viongozi, wastaafu, wafanya kazi, wafanya biashara, wanawake kwa wanaume.

 

Majina yanayojitokeza katika mtandao ulioniathiri mimi ni:

1. Mr. D.A. Odhiambo
2. Mr. George Kachingwe
3. Mr. S.H. ole Sabai
4.Mr. Waltra Harbra
Wengine ni

1. Mr. Mzee Abdala (anajifanya ni Askari wa kitengo cha ukachero Makao Makuu Polisi DSM)- aka James Shebashi



2. Mr. Ephrahim Kajala (aajifanya ni askari upelelezi msaidizi wa 'Mzee Abdala') aka Kalonga Kalonga



3. Mr. Selemani Juma Kaboko - mwenye account NBC na anatumiwa na kundi hili kama mfereji wa kupishia fedha.

Jamaa hawa wanatumia majina ya watu na wanafanya utafiti wa kutosha kama kawaida ya matapeli wa kwenye mitandao. Kwa ujumla wao wanatumia jina la Japan- Tanzania Orphan Project wakipose kuwa inafadhiliwa na JICA. Katika makabrasha niliyoyaona jina hili hili la kampuni feki limetumika kwa zaidi ya miaka mitatu.



Jamani tuwe macho sana na atakayepata habari hii na amtaarifu ndugu jamaa rafiki na mwingine yeyote mwenye mapenzi mema. Kwa upande wangu kikubwa ni kujaribu kuvunja huu mtandao na nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu. Labda ni ndoto lakini nadhani nataka kufanya hivyo nione nitafikia wapi.

Wasaalam

JOSEPHINE LEMOYAN

MATUTA BARABARANI NI SULUHISHO LA AJALI TANZANIA??

Ndugu zangu wapenda maendeleo na mazingira mazuri. Hivi karibuni katika Nchi yetu ya Tanzania kuna ajali nyingi ´sana za barabarani. Hii kweli ni kero kwa Taifa na hasa wale wananchi walioko eneo husika la ajali. Bila kusahau si miaka mingi imepita tangu barabara nyingi na nzuri zijengwe katika Taifa letu. Miaka kama 20 iliyopita zilikuwa mbaya hazipitiki wakati wa mvua na ilikuwa ni kero kweli kweli. Ninatokéa kusini Mtwara, wanaojua wanaweza pata picha halisi.

Tumshukuru Mungu walao barabara nyingi kuu zimejengwa kwa kiwango cha lami na kupitika muda wote. Sasa tatizo linakuja tena. Madereva nao wanakuwa vichaa. Wanaendesha kwa kasi hata magari mabovu kwa sababu tu ya uzuri wa Barabara. Matokeo yake ni ajali za kila siku.

Wananchi nao wanakuja juu. Wanaona njia ya kunusuru maisha yao ni kujenga matuta katika barabara hizi. Waamechukua hatua hata kufunga barabara na kulazimisha serekali kujenga matuta hayo. Mfano´ni majuzi wananchi wa Mkuranga wameamua kufanya hivyo.

Mkuu wa Wilaya akaahidi pale pale kujenga matuta. Wanafunzi wa Chuo kikuu nao walifanya hivyo. Swali langu ni JE KUJENGA MATUTA BARABARA NI SULUHISHO?-

Kujenga matuta barabarani ni kuharibu manthari ya barabara- Kujenga matuta ni kuharibu magari- kujenga matuta ni kuongeza gharama zisizokuwa za lazima katika Taifa letu. Kaangalie matumizi ya Wilaya. Usishangae kuona Sh. Bil. 1 au zaidi zimetumika kujenga matuta barabarani. Kwa nini wasingetumia fedha hizo kununua madawati?-

Kujenga matuta ni kutotumia akili kukabili tatizo. Dereva hana akili mpaka awekewe matuta ili apunguze mwendo!Pendekezo langu.

Ni kufundisha madereva kutumia na kuheshimu ALAMA za barabarani. Kama mahali pameandikwa Km 80, 50, 30 kwa saa wafuate sheria hiyo.

Kama ni pa kusimama wasimame. Mbona kwa wenzetu wanaweza? Wanaweza kwa sababu wanafuata utaratibu na kufuata sheria za Barabarani. Je sisi Watanzania ni wagumu kiasi hicho au hatuna akili mpaka tuwekewe magogo barabarani ndipo tusimamame au tupunguze mwendo?

Katika nchi ya Ujerumani, alama za barabarani, namna ya kutupa takataka katika mapipa ya taka mijini ni somo linalofundishwa darasani. Na wanafunzi wanafanya zoezi hilo kwa vitendo. Hivi wanakua katika hali ya kujua alama hizo na kuziheshimu.

Ujerumani kama alama si ya kijani. Hata kama hakuna gari au mtu, mtu au gari havuki barabara. Anafuata sheria ya Alama. Na iwapo utavunja sheria hiyo hakika adhabu yake ni kali sana. Je serikali yetu imeshindwa kuweka sheria kali na kuzifuata hadi kufikia hali ya kuharibu barabara zilizojengwa kwa gharama kubwa kwa kuweka matuta?

Jamani KUWEKA MATUTA BARABARANI NI KUHARIBU MAZINGIRA.
Mnasemaje?

Slyvanus Kessy

JIHADHARI NA UTAPELI HUU

Imemtokea mwenzetu

Ndugu wapendwa,
Story ifuatayo ni ya kweli maana imenitokea mimi binafsi jana tarehe11/11/2009. Najua kwa kiasi fulani itakuwa inaninizalilisha kwakutokuwa makini lakini naona ni vyema niwashirikishe rafiki zangu ilimsije mkatapeliwa kama mimi na wengine wengi wameshatapeliwa kama vilendugu yake Galeba, laiti Galeba angeweza kutuelezea yaliyomsibu nduguyake labda na mimi ningeweza kuepuka utapeli huu.


Kinchosikitishamatapeli wenyewe ni watu wanaotufahamu vizuri.
Mnamo muda wa saa tano asubuhi nikiwa nyumbani (nipo likizo) nikapokeasimu nisiyoifahamu kutoka kwa mtu ambaye alijitambulisha ananifahamu,na kwa jinsi alivyonitaja kwa jina na career background details zangusikuwa na shaka kwamba hanifahamu.


Mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo:

TAPELI: Mr. Alex Matovu habari za siku nyingi.

Mimi: Nzuri

Tapeli: Vipi bado unafanya kazi Blue Financial Services?

Mimi: Hapana, nani mwenzangu?

Tapeli: John, nilikuwa nafanya kazi Wizara ya elimu, na uliwahikunisaidia nikapata mkopo, ila kwa sasa nipo World food programme,Kigoma kama Chief supplies officer.

Mimi: okay sasa nikusaidie nini John (ukweli nikwamba sikumkumbuka ilakwa kuwa tulikuwa tunatoa mikopo kwa wafanyakazi wa serikali, sikujiuliza sana, after all alikuwa hajasema anachotaka)

Tapeli: Sasa nina issue naomba unisikilize kwa makini, kamaunavyofahamu WFP tunatoamisaada ya vyakula hivyo tuna maghala makubwaya kuhifaadhi chakula, hivyo ili kuhakikisha vyakula haviharibiki huwatuna weka presavative inayoitwa Damoline Liquid solution made inSweeden, hii inapatikana MSD na kwa licensed dealers kama MohamediEnterprises. Kwahiyo tuli float tender mwaka jana na supplieraliyeshinda tulikubaliana anipe 10% lakini baada ya ku supply hayomadawa akanidhulumu na kunitisha kuwa iwapo nitamdai hiyo 10%angeniripoti kwa mabosi wangu. Kwa hiyo sikuwa na cha kumfanya balikusubiri contract yake iishe alafu nimtafute supplier mwingine. Sasandio nikaona nikupigie ndugu yangu maana nakujua wewe hii kazi utawezakuifanya ukizingatia unalipwa cash on delivery!


NOTE: nimeshawahi ku deal na supplies officer wengi hivyo sikuwa nadoubt yeyote, bali nikaona hii is just another deal kama ambazonimeshawahi kufanya successfully.

Mimi: Okay sasa unataka nifanye je?

Tapeli: Unachotakiwa kufanya ni kwenda MSD umuone Dr. Shija, huyundiye mkuu wa hapo na ndiye aliyekuwa supplier wetu wa zamani aliye nidhulumu, sasa kwa kuwa sitaki kumpa kazi tena, wewe uende ujifanyeunaulizia hiyo liquid solution, na u negotiate ujue atakuuziashillingi ngapi. Kwahiyo nakutumia simu yake mpigie muongee akupequotation, alafu akisha kupa bei nipigie ili nikuelekeze cha kufanya.

Basi wandugu nikampigia dr. shija, mwanzoni shija ana hesitatekuzungumza na mimi aki pretend kuwa hapendi kuongea na strangers naakataka kujua namba yake nimeipataje, sasa kwa kuwa siwezi kumwambiaukweli kuhusu aliyenipa namba yake, ikabidi na mimi niwe muongo kwamuda, nika pretend kuwa mimi ni mkulima na nahitaji hiyo presavativekwa ajili ya maghala yangu yaliyopo arusha. Basi akawa na imani nakukiri kuwa anayo stock yakutosha, na hiyo liquid inauzwa kwa pair yachupa mbili zenye ujazo wa 1000mls, kila pair ni 1.2m. Sasa angalianilivyoingia katika mtego, baada ya kunipa bei ni kaomba punguzo naakasema atauza kwa 1million.

Nikafanya kama nilivyoelekezwa na John wa WFP kuwa baada ya kupata beinimjulishe nilivyomjulisha akasema kinachofuata ni kuwa mimi nitauzakwa USD. 1700, na tofauti kwa maana ya faida tutagawana, hivyonisubiri aniunganishe kwa bosi wake for further final details.

Basi wandugu kama mnavyonijua katika issue za fwedha, nikachukuacalculator ya simu ili nijue deal ina shillingi ngapi, helazilivyokuwa nyingi hata calculator iligoma, maana WFP wanahitaji 50pairs @ usd 1700, mimi nanunua kila pair kwa 1million ambayo ni kamausd 770 hivyo difference usd 930 x 50 pairs = USD 46500, ALAFUtunagawana pasu pasu.

Guys you can imagine what was going on in myhead!

Basi kweli muda si mrefu nikapigiwa simu na huyo bosi wake ambaye nimzungu na mazungumzo yalikua kama ifuatavyo:

MZUNGU: This is Mr. Scheinder from WFP, are you the new supplier?

MIMI: YES

MZUNGU: Do you have enough stock of Damoline Liquid solution, we arelooking for 50 pairs?MIMI: Yes I have sufficeint stock

Mzungu: what is your price per pair?

Mimi:$1700

Mzungu: ahaaaaaaaa thats a very good price, do you want to be paid indollars or TZS

MIMI: Dollar of course, you how how unstable the local currency is (Hapo tena na mimi nataka kuonyesha kuwa ni International businessman)

Mzungu: No problem, we have enough dollars, you want to be paid cashor by cheque?

Mimi:Cash

Mzungu: Okay no problem, now listen very carefully mr. new supplier weneed this liquid urgently possibly today, and since you have said youhave enoughstock we are taking off this morning from Kigoma coming to Dar, pleasearrange for the transport to take us to Movenpick, we will pay usd.200 for your fuel, but most importantly make sure you bring one pairof the sample with you.

Mimi: No problem at all I have been in this business for quitesometime now you can be sure everthing will be fine.

Masikini bila kujua nimeingizwa kingi, nikachukua cheque book,nikaandika cash withdraw 1million ili nikanunue sample yakwendakuwaonyesha wateja wangu.

Baada ya kutoka bank nikampigia dr. shijaili aniuzie hiyo sample, akasema kwa sasa ametoka ofisini ila sampleanazo katika gari na alikuwa anaelekea Mwananyamala hosp, thenMagomeni alafu Muhimbili, hivyo tukutane Magomeni hosp.

Yaani jinsinilivykuwa naendesha gari basi hata kama ni mashindano ningewezakushinda, basi mimi mbio mpaka magomeni hosp namsubiri dr. shija.

Nikampigia akasema yupo ndani hospitalini na yupo na mabosi wakeasingeweza kutoka ila anamtuma kijana wake nimpe hizo fedha na yeyeanipe hizo dawa, kweli ikawa hivyo kijana akaja akaingia kwenye garinikamwambie anipe hizo sample kwanza nikazisoma ziko exactly kama WFPwanavyotaka! NIKAKABIDHI HELA 1 MILLION.

Bila hata aibu yule kijanaakaniomba 50,000/= nikamwambie asijali maana deal kubwa itakamilishwasaa nane.

Kwa kuwa wageni wangu walishaniambia niwaaandalie usafiri, nikampigiadreva tax wangu aje airport saa nane, nikamuuliza bei kutoka airportmpaka movenpick ni ngapi akasema 25,000 nikamwambia usijali ntakupa50,000/=!!!!!!!!!!!!! (kumbuka mimi ntalipwa usd 200 ya usafiri).

Basi mimi mbio nikaenda airport terminal one kusubiri ndege ya WFP ilitumalize biashara, nilipofika kuulizia reception nikaambiwa hakunakitu cha namna hiyo na mimi ni mtu wa 10 kutapeliwa, basi tenanikajirudia kimya kimya. Nikaenda kula chefs pride nikamsimulia jamaammoja yaliyonisibu, kabla sijamaliza akasema hata ndugu yakeametapeliwa wiki iliyopita, nikampigia Galeba akasema yeye jamaa yakealipigwa 3.5m last week.


Edwin

Monday, November 16, 2009

MAISHA BORA KWA MTANZANIA???!!!!

Nimejaribu kuwanaliangalia hili neno "maisha bora kwa mtanzania" kwa uelwa wangu mdogo ni kama tusi au kejeli kwa kiongozi wa serikali kuliongea mbele yangu.

Kuna wizara ya mipango nanini sijui au kama haipo ila najua iko wizara inae waziri atleast inafanya mipango ya mustakhabari wa maendeleo ya nchi yangu, kila siku wingu la umasikini linazidi kuwa jeusi na wahusika hawawajibiki.

Inawezekana maisha bora ni kulala kwenye nyumba nzuri, kuendesha gari zuri, kula vizuri.... nk.

Sawa lak9ini vinatoka wapi? Karume marehemu alijenga nyumba kwa ajili ya wananchi wake, kunasehemu siikumbuki jina watu wanapikia kuni ghorofani na nyumba hazijulikani rangi yake ya kwanza ilikua ni ipi.

Zilijengwa kwa nguvu ya wananchi huku kukiwa na ulazimishwaji ndani yake, leo ukienda ukamtoa yule mwananchi atalaani kama nini.

Tunapoongelea maisha bora ya mtanzania nilitegemea nisijengewe nyumba na serikali ila niwekewe mazingira bora ya kunifanya nishamiri kimaisha.

Ninaomba mtu aniwekee ufafanuzi juu ya kilimo kwanza. Kama nalo ni moja ya kuelekea kweye maisha bora ya mtanzania well labda japo sina uhakika kwani yalikuwepo maazimio yahusuyo kilimo miaka mingi sana na sidhani kama linakitu kipya toka yale yaliopita.

Hivi ukiniambia nilime, sawa utanipa matrekta ambayo nasikia yule SPONSOR wa harusi ya waheshimiwa wawili kadaka tenda kunakitu hapo? Mkulima wa karafuu lazima awe na sababu ya kulima kama utamuhakikishia kuwepo kwa soko na bei nzuri ya mazao yao, je lipo hilo?

Japo soko ni kitu muhimu kwa mkulima lakini barabara za kufika kule alipo zipo? Nchi ina njaa kwa sasa lakini mpanda kunachakula kingi sana halafu reli ndo tumeiua. Tatizo kubwa linakuja nikutoona mipango mizuri endelevu inayokwenda sambamba na neno lenyewe "maisha bora kwa mtanzania".

Sekta binafsi ni sehemu nzuri sana ya kuleta maendeleo kwa nchi, tunahangaika na wawekezaji wa nje wakati tunashindwa kuwafanya wawekezaji wa ndani kukua na kuleta ushindani.

Hivi migodi yote kweli ni sahihi kuwapa watu wa nje? labda migodi ni kitu kikubwa na haya mashirika yaliouzwa kinyemela.

Kama mwekezaji wa ndani hana msaada toka kwa serikali yake mwenyewe hayo maisha bora yanakujaje? Fikiria mtu kaweza kuanzisha kampuni, kajitahidi kakusanya human resources nzuri tu anatafuta fursa ya biashara anashindwa kwa kukosa mtaji.

Tanzania investment benki (TIB) ipo haina msaada wowote kwanza inanichefua sana utendaji wake. Nilitegemea kuwa nimekuja na wazo liko verypositive napata support ya serikali, hata kama nitachukua mtaji toka TIB wakaweka mtu wao wa kusimamia mapato ya kampuni yangu mpaka deni lao likaisha sijali lakini hata hilo linashindikana.

Watanzania wako very creative ila system mbovu kiasi kwamba wanakuwa nafrustrations halafu mtu anasimama na kunihubiria maisha bora kwa mtanzania.

Kuna haja kubwa sana ya kufanya mabadiliko makubwa kwenye muundo wa ukusanyaji mapato kwani mapato mengi sana yanapotelea mikononi mwa watu na serikali kushindwa kutoa hudumua kwa wananchi.

Muundo wa vyombo vya usalama na sheria hautoi muelekeo mzuri wa hili neno "maisha bora kwa mtanzani" kama rushwa itandelea, sheria hazifuatwi ni ngumu sana.

Uendeshaji wa mambo kwa kuheshimu taaluma ni kitu kilichokwisha poteza kabisa maana, mfano rahisi waziri anapotoa agizo bara bara ziwekwe matuta, mtaalamu akatekeleza.

Nimeshangaa TANROAD wamekubali hilo pia, je sheria za barabarani zingekuwa zinafuatwa tungekuwa na hofu ya kupoteza maisha ya watu? Sipendi kusikia mtu anaongelea maisha bora kwa mtanzania kwani ni kejeli na hata aneliongelea hajui maana yake.

Jovias Mwesiga
wanabidii@googlegroups.com

ATM ZINAPOKUWA KERO



Hivi hizi ATM zilizowekwa katika mabenki ni mchezo wa kuigiza ama ni nini hasa?Mfano hapa Morogoro toka Alhamisi iliyopita ATM za bank ya NBC zilikuwa hazifanyi kazi hii si mara ya kwanza ni mara nyingi tu na si tatizo hili linatokea unaenda kuchukua pesa yako kwa ajili ya matumizi unakuta mstari mrefu ama haifanyi kazi si NBC tu hata NMB.

Mfano hapa Morogoro kuna ATM zisizopungua tano za bank ya NBC cha kushangaza ni kwamba unaweza kuta zote hazifanyi kazi,kilichonikera zaidi siku ya alhamisi ATM palepale bank ilikuwa haifanyi kazi na ndani ya bank walikuwa wanapokea pesa tu na si kuchukua pesa,sasa pesa za wananchi ,ambazo hata hizi kazi zetu za kipato cha chini tunaambiwa kupokelea banki inakuwaje???

Nilishangaa kukuta wafanyakazi wa kampuni moja ya Tumbaku wakiwawamesubiri mshahara wao wa siku 15 toka asubuhi na mimi nilifika hapo saa 10 jioni.

Ninavyofahamu kuna watu wa IT katika mabenki yetu na wamepewa majukumu ya kuhakikisha ATM zinafanya kazi na wanalipwa pesa nyingi je wako makini na kazi yao kweli??? na Je hizi ATM ziko katika ubora unatakiwa kweli ama ni danganya toto????