Friday, November 6, 2009

TANZANIA, NCHI YA AMANI...

Shule za Vijijini


Madarasa ya shule za vijijini

HAPA CHINI

Jengo la Ubarozi wa Tanzania huko Washington






Ofisi zetu za Bunge

Kuna cha kuongeza?

Thursday, November 5, 2009

NDOO ZA PLASTIK ZINAPOKUWA MADAWATI

Afisa wa benki ya Kenya Commercial Bank kitengo cha Jamii tawi la Morogoro, Herrieth Gilbet kulia akimkabidhi sehemu ya madawati Afisa Elimu Ngazi ya Sekondari Manispaa ya Morogoro Jasper Bitwale wakati wa hafla ya kupokea msaada wa madawati yaliyotolewa na benki hiyo shuleni hapo katikati ni Mkuu wa Shule hiyo, Flora Masoy

Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya Mgulasi katika Manispaa ya Morogoro, Flora Masoy, kulia akimtembeza Afisa wa benki ya Kenya Commercial Bank kitengo cha Jamii tawi la Morogoro, Herrieth Gilbet na kujionea hali halisi ya jinsi wanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule hiyo wanavyokalia ndoo za plastiki muda muda mfupi kabla ya benki ya KCB kutoa msaada wa madawati yenye thamani ya zaidi ya sh Milioni 5.

Wanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari ya Mgulasi katika Manispaa ya Morogoro, wakimsikiliza kwa umakini mwalimu wa darasa hilo Lucy Ngowi (hayupo pichani) wakati wa somo la kuandika barua huku wakiwa wamekalia katika ndoo za plastiki muda mfupi kabla ya benki ya KCB kutoa msaada wa madawati yenye thamani ya za sh Milioni 5.(Picha na Juma Mtanda)

Wednesday, November 4, 2009

USHAURI KWA WAANDISHI

Kwa sisi ambao tuko "ughaibuni" na huja nyumbani mara kwa mara, tunachoka sana kusoma "habari mbaya" tu kutoka nyumbani! Tunafurahi zaidi kusoma habari nzuri; ambazo tunajua ni nyingi huko nyumbani! .

Kuanzia oneni link hii ya "Goodnews Toronto" - Kuhusu Mtoto Stephano kutoka Mbeya, Tanzania. http://www.goodnewstoronto.ca/heroes.html.
Ahsateni. Mabula

Monday, November 2, 2009

NICO NA ELIZABETH WALIPOMEREMETA







Mdau wa blog hii Nico Mujaya "Chifu" hivi karibuni aliamua kuiaga kambi ya waseja na kufunga pingu za maisha na Elizabeth Mustapha,ndo ilifungwa katika Kanisa la Waadventista Wasabato Kirumba,Mwanza na sherehe ya kuwapongeza iliyofanyika kwenye ukumbi wa New Mwanza Hotel jijini Mwanza.

URAFIKI WA NYOKA NA BINADAMU!! DU!!


WEWE UNAWEZA?

Friday, October 30, 2009

MUARGENTINA ATAKAYE PAMBANA NA CHEKA AFAHAMIKA

Cheka akiwa Mazoezini katika gym ya Simba Oil Morogoro

Bondia Enrique Areco wa Argentina ndiye atakayezipiga na Bingwa wa dunia wa uzito wa middle anayetambuliwa na Chama cha Ngumi za Kulipwa cha UBO,Francis Cheka kwenye uwanja wa Uhuru desemba 19 mwaka huu huko jijini Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Rais wa Shirikisho la Masumbwi Tanzania PST Emmanuel Mlundwa alisema jana kuwa Cheka atawania ubingwa wa Kamisheni ya Dunia ya ngumi za kulipwa au World Boxing Commision WBC ambao unashikiliwa na Areco.
Mtandao wa www.boxrec.com umemwelezea Enrique Areco aliyezaliwa mwaka 1964 kuwa ameshinda mapigano 43 ambapo 13 ni kwa KO,akiwa amepoteza michezo 15 ambapo 6 ikiwa ni kwa KO na kutoka sare michezo 7
Mtandao huo pia unamwelezea Francis Cheka kuwa bondia huyo aliyezaliwa 1982 na kuanza kucheza mpira wa miguu akiwa kipa wa timu ya Nondo FC ameshinda mapambano 18 ambapo 12 ikiwa ni kwa KO na kupoteza 6 ikiwa ni kwa KO kwa michezo 3 na kutoka sare pambano moja.

BAO NAO WAPO SHIMIWI MOROGORO

Mchezaji wa mchezo wa bao katika wizara ya Mambo ya Nje Raphael Barua kushoto akimwangalia kwa umakini mpinzani wake, Lameck Mboje kutoka Tamisemi akitandaza kete wakati wa mashindano shimiwi kwa mchezo huo uwanja wa Jamhuri mjini hapa, Lameck Mboje kulia alishinda kwa bao 1-0.(Picha na Juma Mtanda)