Wizara
ya Ujenzi inapenda kutoa taarifa kwa Umma kwamba, Mei 22, 2013
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete atakuwa mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa miradi ya
ujenzi wa barabara kama ifuatavyo:-
1) Tarehe 22 Mei, 2013 Asubuhi kuweka jiwe la msingi sehemu ya Dodoma – Fufu Escarpment (km 93.8) katika eneo la Dodoma Mjini.
2) Tarehe
22 Mei, 2013 Mchana kuweka jiwe la msingi sehemu ya Fufu Escarpment –
Migori (km 70.9) na Migori – Iringa (km 95.3) katika Kijiji cha Migori
Wilayani Iringa Vijijini.
Barabara
ya Iringa - Dodoma ni sehemu ya barabara muhimu ijulikanayo kama “Great
North Road” inayoanzia Capetown Afrika ya Kusini hadi Cairo, Misri
kupitia Tanzania. Nchini Tanzania inaunganisha Miji ya Tunduma (mpakani
na Zambia), Mbeya, Iringa, Dodoma, Arusha na Namanga (mpakani na Kenya).
Mradi
huu ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha
miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara na unalenga kupanua fursa za
kiuchumi na kibiashara kwa wananchi, na kati ya Tanzania na nchi jirani
za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC). Kwa njia hii, barabara itakuza uchumi wa wananchi na
Taifa kwa ujumla.
Taarifa hii imetolewa na;
Balozi Herbert E. Mrango
KATIBU MKUU
WIZARA YA UJENZI
Tuesday, May 21, 2013
Monday, May 20, 2013
UZINDUZI WA DVD MWONEKANO NAMBA MBILI YA MBIU KWAYA HUU HAPA
Mbiu Kwaya toka Kanisa la Waadventista Wasabato Tandale jijini Dar es salaam inataraji kufanya uzinduzi wa DVD mwonekano namba 2 waliyoipa jina la Fikiri Mwenyewe,uzinduzi utakofanyika Juni 2,2013 katika ukumbi wa Delux Hall Sinza jijini Dar es salaam,Tanzania,kuanzia saa 6 mchana.
Uzinduzi huo uliodhaminiwa na Excellent Pro utawahusisha pia waimbaji wa Sonda ya Dilu,Kurasini SDA Choir,Angaza Kwaya,Familia ya Injili
Friday, May 17, 2013
TAMASHA LA UIMBAJI LA VOCAL PRAISE NA GOSPEL FLAMES HILI HAPA
Thursday, May 9, 2013
Wednesday, May 8, 2013
TAMASHA LA FRIENDS OF JESUS CHOIR HILI HAPA
Friends
of Jesus Choir (FoJ) ya Rwanda inataraji kufanya tamasha la uzinduzi wa toleo lao namba saba walilolipa jina "SHEPHERD OF MY SOUL". likiwa na nyimbo 5 za kinyarwanda , 6za kiingereza na mmoja wa kiswahili.
Waimbaji wengine watakaokuwepo ni kwenye uzinduzi huo utaofanyika kwenye Hoteli ya Serena,Kigali Rwanda Mei 18,2013 ni The Voice toka Dar es salaam, Tanzania,Shower Power toka Zimbabawe na Trevor toka Marekani ambaye ni Profesa wa Muziki wa Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki na Kati cha Kanisa la Waadventista Wasabato kilichopo nchini Kenya
Waimbaji wengine watakaokuwepo ni kwenye uzinduzi huo utaofanyika kwenye Hoteli ya Serena,Kigali Rwanda Mei 18,2013 ni The Voice toka Dar es salaam, Tanzania,Shower Power toka Zimbabawe na Trevor toka Marekani ambaye ni Profesa wa Muziki wa Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki na Kati cha Kanisa la Waadventista Wasabato kilichopo nchini Kenya
WAZIRI MKUU WA TANZANIA AMEONYA KUTOSHABIKIA MAAFA
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewaonya baadhi ya watu wanaofanya ushabiki wa kisiasa kwenye tukio la mlipuko wa Arusha na kuwataka wasitumie tukio hilo kujipatia umaarufu na badala yake watumie fursa hiyo kuwafariji walioathirika na kuwa watulivu hadi suala hilo lifikie hatma yake.
Waziri Mkuu amesema tukio hilo ni kubwa, na kitendo hicho ni kibaya kinachostahili kulaaniwa vikali kwa hiyo haifai watu wachahe kujipatia umaarufu kupitia tukio hilo.
Ametoa kauli hiyo jana asubuhi (Jumanne, Mei 7, 2013) wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwatembelea ili kuwajulia hali majeruhi waliolazwa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, jijini Arusha.
Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na hali ya utulivu wa wananchi wa Arusha na hasa waliokaribu na Kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, kufuatia mlipuko wa mabomu uliotokea Jumapili iliyopita, Mei 5, mwaka huu. Alisema ameguswa pia na hali ya matibabu inayotolewa kwa majeruhi katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, jijini Arusha.
Waziri Mkuu alikatisha shughuli za Bunge juna mchana na kuelekea Arusha. Mara baada ya kuwasili KIA juna jioni, Waziri Mkuu alikwenda moja kwa moja Parokia ya Olasiti ili kujionea hali halisi na kuwapa pole wamunini wa Kanisa hilo.
Baadaye alikwenda kumjulia hali Askofu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu Josephat Lebulu pamoja na Balozi wa Vatican, Mhashamu Askofu Fransisko Padilla ambako alifanya nao mazungumzo na kuwahakikishia viongozi hao kwamba Serikali itafanya kila iwezalo hadi iwabane wahusika.
Akiwa hospitali ya Mount Meru leo asubuhi, Waziri Mkuu alimweleza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Dk. Frida Mokiti kuwa asisite kuwasiliana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Magesa Mulongo endapo hali ya majeruhi itabadilika na watahitaji matibabu zaidi.
Katika ziara hiyo fupi, Waziri Mkuu alikabidhi vifaa vyenye thamani ya sh. milioni 23.3 ambavyo ni dawa na vifaa tiba kwa uongozi wa hospitali hiyo ambavyo vilitolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) chini ya uhamasishaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kukabidhi misaada hiyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Bw. Lazaro Nyalandu alisema juzi (Jumatatu, Mei 6, 2013), TANAPA ilitoa mablanketi 50 hospitali hiyo na kwamba wafanyabiashara wa sekta ya utalii wa mjini Arusha wamejipanga kutoa msaada zaidi ili kuisaidia hospitali hiyo kumudu kuwahudumia majeruhi wa mlipuko huo.
Hadi sasa, watu watatu wamepoteza maisha kutokana na mlipuko huo ambapo watu wanane wamekamatwa na kuhojiwa na polisi. Kati yao, wanne ni raia wa Saudi Arabia na waliobakia ni wakazi wa Arusha. Polisi bado wanaendelea na uchunguzi wa tulio hilo.
Akitoa taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Arusha alisema wagonjwa watatu wana hali mbaya ambapo mgonjwa mmoja yuko Muhimbili na wawili wako hapo hapo Mount Meru.
“Watu 66 waliathirika na mlipuko huo, watatu wamefariki na kati ya wagonjwa 63 waliobakia, wagonjwa 24 wamesharuhusiwa kurudi nyumbani, waliobakia wanaendelea kupatiwa matibabu,” alisema. Waziri Mkuu amerejea Dodoma mchana huu.
IMETOLEWA NA: OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P 980,
DODOMA. JUMANNE, MEI 7, 2013.
Saturday, May 4, 2013
UZINDUZI WA DVD YA RESTUTA WILLIAM MWACHULA KUFANYIKA KESHO MEI 5,2013 TAZARA DAR ES SAALAM
Mtangazaji akiwa na Waimbaji wa Victory Singers toka Mwanza,Joseph Oola,Namsifu Makacha toka Arusha na Restuta Mwachula baada ya kipindi cha Lulu za Injili leo Morning Star Radio waimbaji hawa wataimba kesho Mei 5,2013 katika uzinduzi wa Dvd ya kwanza ya Restuta Mwachula toka Dar es salaam utakaofanyika katika ukumbi wa TAZARA barabara ya Nyerere kuanzia saa sita mchana
Waimbaji wengine watakaokuwepo kwenye uzinduzi huo ambao utachangia sh.3000 za kitanzania ni Angaza SDA Choir,Mbiu Kwaya,Ulongoni A,Acacia Singers na Sonda ya Dilu .
Subscribe to:
Posts (Atom)








